Inatafuta...

KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA - 12

KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA -12
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Karibu utufollow kwenye Twitter Maana hadithi zote zitaanza kurushwa huko @swahilifive
Web: www.swahilifive.com

IIPPOISHIA
“Ndiyo maana yangu, itakuwa si mbaya sana,” baba Joy alisema huku akionesha dalili za kuchanganyikiwa. Alimini kuwa, endapo ataiacha simu yake pale ndani akipigiwa na Helena au Fuko hatajua.

Yule binti aligeuka kurudi ndani akimaanisha anakwenda kuchukua chaja. Baada ya muda alirejea…

“Hii, si utairudisha mwenyewe..?”

“Usajali binti, nitairudisha mimi mwenyewe, nakushukuru sana binti yangu…”

“Usijali baba.”

Baba Joy alitoka haraka na chaja hiyo hadi kwenye ule mgahawa…

“Ee bwana nimebahatisha chaja, naomba nichomekee kwenye soketi yenu basi.”

Chaja ilipokelewa, ikapelekwa kwenye soketi huku baba Joy akiwa amerudi kwenye kiti alichokaa na kuendelea  kunywa soda yake.



***

Mama Joy na mzoa taka waliongea mengi kuhusu chumba cha kijana huyo, alimuahidi kumnunulia godoro, kitanda, kabati la ngu, meza, redio, tivii na kapeti kubwa chini…

“Lakini nakuonya, usije ukakifanya chumba cha kuingiza malaya wako…”

“Haitawezekana mupenzi, mimi nakupenda wewe, kama hivi unaniwezesha, unanitengenezea maisha…”

“Hapo umesema, mimi sitaki kabisa mwanamuem malayamalaya.”

Mama Joy aliposema hataki wanaume malayamalaya, mzoa taka alitamani kusema…

“Mbona we malaya tu.”

Mama Joy akijua muda unakwenda, alianza kwa kumshikashika mzoa taka sehemu mbalimbali za mwili…

“Sasa kijana ukiwa unajua tutakutana uwage unaoga hata kidogo jamani…”

“Leo dawasa walizuia maji…”

“Uwe unajitahidi kuhifadhi, sawa?”

“Sawa mupenzi…”

“Halafu mi sitaki uwe unaniita mupenzi, we ita mpenzi tu nitakuelewa,” alisema mama Joy huku akiendelea kumshikashika kijana huyo, mwili ulimsisimka, damu zilimtembea kwa kasi, akaanza kuhisi kuzimiazimia kwa raha na yeye akapeleka mkono kwenye ‘nido’ la kulia la mwanamke huyo, mama Joy akaruka kidogo...

“Wao, umejuaje kijana wangu. Hapo uliposhika ndipo penye transifoma,” alisema mama Joy.



***

Helena aliamua kuweka wazi kwa Fuko akiamini hata yeye amekatiwa kitu kidogo chake…

“Mimi alinipa hela, lakini hapa hoja si hela bali ni kumpata bosi ili tumwambie mzoa taka yumo chumbani mwako, tena kitandani,” alisema Helena…

“Ni kweli, ana simu mbili, lakini ile simu moja sijui inatumia namba gani?” alisema mlinzi. Walipiga plani ya kwenda kwa mama Joy ili wakaombe namba lakini wakaona haiwezekani…

“Atakuuliza unataka namba yake hii ya nini? Halafu tena mfano akikupa halafu mumewe akarudi sasa hivi na kumfumania si atajua ni sisi kwa sababu tuliomba namba…”

“Ni kweli, itakuwa ngumu, sasa tufanyeje?”

“Mh! tuendelee kumpigia, itakuwa simu imeisha chaji, akiwasha tu tutampata tutamwambia…”

“Au tumtumie meseji, wewe mtumie na mimi ili akifungua simu na kukutana nazo atajua kumbe tulimtafuta wote.”



***

Kule kwenye mgahawa, mara muuza mgahawa alitokea akiwa ameshika ile chaja aliyokwenda nayo baba Jy pale…

“Bwana vipi, tayari mara hii?” baba Joy aliuliza akiwa na uso wa shauku…

“Mzee hii chaja kumbe ni ya pini kubwa, sijui itakuwaje?”

“Haa!” baba Joy alihamaki, picha ya mzoa taka na mkewe mama Joy ilimwingia hivihivi anaona kwa sababu tu ya kukosa mawasiliano…

“Ile simu ingekuwa nzima ningeitumia, sasa…”



***

Kule chumbani, mama Joy na mzoa taka mchakato ulikolea kupita kawaida. Mapenzi yalikuwa motomoto, kila sehemu ya kitanda ilitoa mlio wa masikitiko kwa kulemewa na uzito wa walio juu.

Mzoa taka alijituma kuliko jana na juzi. Mama Joy alikuwa mtu wa ‘kulalamika’ tu kama yuko na mumewe. Hakujali kwamba baba Joy angeweza kurejea nyumbani hapo ghafla na kuwanasa.

Mlinzi, baada ya kumkosa baba Joy kwenye simu alifanya doria. Alikuwa akienda ndani na kusimama kwenye mlanngo wa mama Joy kisha kurudi getini. Kuna wakati alipokuwa amesimama hapo mlangoni, Helena naye alitokea…

“Bado wapo?”

“Bado, tena bosi anapiga kelele sana, huyu mwanamke anatafuta matatizo,” alisema mlinzi.



***

“Basi jamani nawaombeni nipe simu yenu mi niweke laini yangu mara moja, kuna mtu nataka kuwasiliana naye dakika moja tu,” baba Joy alimwambia yule mwenye mgahawa ambaye naye alitoa laini na kumpatia simu yake.

Baba Joy aliweka laini kwenye simu hiyo na palepale meseji zikaanza kumiminika kwa wingi.

Mapigo ya moyo yalimwenda kwa kasi huku akiwa kama anazisoma meseji hizo kwa hisia kabla ya kuzifungua…

“Bosi hupatikani kwenye simu, umezima. Mzoa taka ndani ya nyumba hapa.” Hiyo ilikuwa meseji kutoka kwa Helena…

“Bosi, mwizi wako keshaingia sasa, kazi kwako ukichelewa utamaliziwa uhondo wote ohooo.” Huyo alikuwa mlinzi.

Baba Joy hakutaka kupoteza muda kwa kusoma meseji nyingine, alimpigia Helena…

“Bosi yumo bado yumo chumbani,” alisema Helena.

Baba Joy alikata simu. Kwa machungu na maumivu ya wivu alijikuta akitaka kuondoka na simu ya watu…

“Sasa mzee wangu mbona unaondoka na simu halafu hii chaja vipi, umeazimia wapi? Soda pia hujalipa mzee wangu.”

“Ooo, sorry. Chaja ya nyumba ya pili hapo, simu yako hii, samahani kwa kutolipa,” alisema baba Joy huku akitoa noti ya shilingi elfu kumi ambayo hakusubiria chenji.

Aliingia ndani ya gari lake na kuondoka kwa kasi kuelekea nyumbani kwake. Barabarani nusura agonge magari mengine. Akili yake ilikuwa haimwambii nini cha kufanya baada ya kufika huko…

“Hivi nikiwakuta laivu niwafanyaje? Niwaue wote, nimuuze yule mshenzi, niwatoa nje na kuwatembeza uchi au? Nitajua hukohuko,” alisema moyoni baba Joy. Hapo alikuwa akikata kona kuingia barabara inayoelekea kwake.

Alipofika getini hakutaka kupiga honi. Aliegesha gari na kushuka akiacha mlango wazi.

Bahati njema kwake alikuta geti liko wazi, akazama ndani na kumwona mlinzi akitokea ndani…

“Bosi wapo chumbani,” mlinzi alimwambia kwa sauti ndogo. Baba Joy alisimama kwanza na kukumbuka bastola ameiacha kwenye gari. Alirudi mbio, akaichukua na kwenda ndani. Alitembea kwa mwendo wa kunyata wakati anaukaribia mlango wa chumbani.

Ulikuwa wakati mgumu sana kwake, mapigo ya moyo yalimwenda kwa kasi zaidi, hakauwa akiamini kama kweli mkewe, tena wa ndoa anaweza kufanya tendo lile.

Baba Joy aliamini akigonga mlango kwa nguvu linaweza kutokea lolote, hivyo aliamua kugonga polepole…

“Ngo ngo ngooo…”

Kule chumbani, mama Joy hakusikia mlango ukigongwa, lakini mzoa taka wake alisikia…

“Mmm…mlango unagongwa mupenzi…”

“Mlango unagongwa! Kweli..?”

“Ngo…ngo…ngo…”

“Nani?” mama Joy aliulizia kwa ndani tena akitumia sauti yenye hasira ya kero.

Baba Joy alishika kitasa na kukichezesha juu na chini mara kadhaa…

“We nani? Helena.”

Jiko halikuwa mbali sana, baba Joy akaenda kumchukua Helena…

“Akiuliza nani, mwambie mimi. Nataka ajue ni wewe kisha aje kufungua akutana na macho yangu,” alisema baba Joy. Kwa kiherehere, mlinzi naye alichomoka kwenye lindo lake na kwenda ndani kujua kulikoni, wakakutana wote watatu pale mlangoni…

“Ngo ngo ngo,” aligonga tena baba Joy…

“Helena…”

“Abee bosi…”

“Unasemaje…?”

“Nina shida bosi…”

“Shida gani, kila kitu si kipo..?”

“Mwambie kuna wageni,” baba Joy alijikaza kiume, alimnong’oneza Helena…

“Kuna wageni mama, ndiyo maana nimekuja kukugongea…”

“Kuna wageniu..?”

“Ndiyo…”

“Wametokea wapi..?”

“Mimi sijui…”

“Wanaume wanawake..?”

“Mchanganyiko.”

Mama Joy aliacha maswali, ilimaanisha anatoka kitandani ili kutoka kwenda sebuleni.

Mara, mlango ulisikika ukifunguliwa kwa ndani…

“Hao ni wageni gani wanaokuja bila…haaa! Mungu wangu eee,” mama Joy hakumalizia kusema baada ya kufungua mlango na kukutana na sura ya mumewe, mlinzi na Helena…

“Rudi chumbani, malaya mkubwa wewe…unawezaje kufanya uchafu huu. Mbuzi we,” alifoka baba Joy huku akimsukuma mama Joy ambaye aliangukia ndani…

“Wewe mbwa wewe,” alisema baba Joy akiwa amemnyooshea bastola mzoa taka…

“Mzee samahani mzeee, usinie mzee wangu. Samahani sana mzee.”

“Wewe unachotakuwa kukifanya ni kusali sala yako ya mwisho na si vinginevyo. Afadhali niwaue na mimi nikafungwe ndiyo itakuwa furaha yangu kubwa, wanyama nyinyi.”

Mzoa taka aliachia haja ndogo pale kitandani. Mama Joy alipoteza fahamu, mlinzi alimkejeli mzoa taka…

“Nilikwambia bwana, acha mali za bosi wangu hukutaka kunisikia, unaona sasa yamekukutana makubwa mchafu kunuka we…”

“Mzee nisamehe mimi sawa na mtoto wako wa kumzaa,” alisema mzoa taka baada ya kumwona baba Joy kaielekeza bastola uswa wake…

“Mzee wangu nisamehe mimi ni mtoto wako mzee…”

“Wewe ni mtoto wangu nilizaa na mama yako yupi? Na kama ni mwanangu iweje ulale na mama yako..?”

“Ni shetani tu.”

Baba Joy alijizuia sana. Ilibaki kidogo tu amlipue kwa bastola, lakini alipowaza kuhusu mali zake, utajiri wake akasikia uchungu nazo. Alijua akifanya hivyo atakwenda kuishia jela. Akasikia sauti ikisema masikioni mwake…

“Unadhani ukienda jela nani atasimamia maliz zako?”
ITAENDELEA SIKU YA KESHO


Karibu utufollow kwenye Twitter Maana muendelezo wa hadithi hii utaanza kurushwa huko @swahilifive
Twitter:www.twitter.com/swahilifive
JE NINI KITAENDELEA ...USIKOSE...SEHEMU YA ....13... 
Kuwa na mimi hapa tena siku ya Kesho itaendelea.....
 

Changia Maoni Yako Hapa

3 comments

Asante kwa Muendelezo

Reply

Ni Tamu sana @ Bongo Choice

Reply

Tuko Pamoja Sana

Reply

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright Bongo Choice | Modified By Bongo Choices
Back To Top