Mama kijacho ambaye ni msanii wa filamu, Aunt Ezekiel juzikati
alinaswa akiwa kliniki huku akiwa amevaa vazi la baibui ambalo
linamuonesha macho tu, maarufu kama vazi la kininja.
Hata hivyo, wakati akitoka kwa daktari, mwandishi wetu aligundua kuwa aliyekuwa akimuona mbele ya macho yake ni Aunt na ndipo alipomfuata na kumuuliza kulikoni.“Nimechoka kuangaliwaangaliwa, yaani mimba yangu imekuwa kama kitu cha ajabu, kila ninapopita watu macho kodooo, ndiyo maana nimeamua niwe navaa hivi ninapokuwa kwenye maeneo yenye watu wengi,” alisema Aunt.
Msanii wa filamu, Aunt Ezekiel akiwa amevaa vazi la baibui ambalo linamuonesha macho tu, maarufu kama vazi la kininja.
Paparazi wetu akiwa kwenye majukumu yake, ghafla alimuona staa huyo
ambaye ni wa kujifungua leo au kesho akiwa kwenye vazi hilo katika
Hospitali ya Penisulla iliyopo Msasani jijini Dar, hali iliyosababisha
watu kutomtambua.Hata hivyo, wakati akitoka kwa daktari, mwandishi wetu aligundua kuwa aliyekuwa akimuona mbele ya macho yake ni Aunt na ndipo alipomfuata na kumuuliza kulikoni.“Nimechoka kuangaliwaangaliwa, yaani mimba yangu imekuwa kama kitu cha ajabu, kila ninapopita watu macho kodooo, ndiyo maana nimeamua niwe navaa hivi ninapokuwa kwenye maeneo yenye watu wengi,” alisema Aunt.
Post a Comment