Inatafuta...

Magufuli Aigeuzia Kibao Taasisi ya Utafiti Iliyompa Ushindi wa Urais..Adai Amepunjwa Asilimia

Kahama. Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amesema waliofanya utafiti wamempunja asilimia kwani ana uhakika wa kushinda kwa asilimia 95 na si 65 kama zilivyotajwa kwa kuwa wananchi wanampenda, naye yuko tayari kufanya kazi ili kuwaletea maendeleo.

Akizungumza jana mjini Kahama, Dk Magufuli alisema: “Wapo wanaosema nimeshinda kwa asilimia 65, mimi ninasema nitashinda kwa asilimia 95, ninachoomba mjitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura ili nitangazwe mshindi, ninawaahidi kwamba nitawatumikia na kujenga Tanzania mpya.”
Hivi karibuni, taasisi ya Twaweza ilitoa utafiti wake uliompa nafasi ushindi wa asilimia 65 huku mpinzani wake, Edward Lowassa akipata asilimia 25 na mgombea wa ACT –Wazalendo akipata asilimia 0.3.
Baadaye, taasisi ya Ipsos (Synovate) ilitoa utafiti wake ukionyesha kwamba alishinda kwa asilimia 62 huku Lowassa akipata asilimia 31 na Anna Mghwira akipata asilimia 0.3.

Changia Maoni Yako Hapa

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright Bongo Choice | Modified By Bongo Choices
Back To Top