Kitanzi, Kisu au Bastola - 02
Credit : 2jiachie
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA
TARATIBU zimwi la upweke likamzonga na kuushinda kirahisi ustahimilivu wa moyo wa Dedan. Kama mfungwa kwa mawazo yake akajikuta hajielewi kabisa. Kichwani akiwaza mara ya kwanza alipoongea na Caro kwa njia ya simu…
ENDELEA SASA...
“Mungu wangu! Msichana mrembo wa ajabu huyu,” alisema moyoni Dedan. Akakumbuka pia alipoamua kumfungulia kurasa mpya za mapenzi ndani ya kuta za moyo wake.
Alikumbuka vyema kila zuri walilofanya pamoja, wakicheza baharini na kurushiana mito kitandani. Walilishana chakula na kubusiana kimahaba.
Lakini hayo yote yalitoweka ghafla baada ya kukumbuka sauti kali ya Carolina kwenye simu ikimtosa bila huruma na pasipokuwa na sababu yoyote. Akasikia sauti nyingine ya mwanaume wake wa sasa ikimchimba mkwara kwamba atakiona cha mtemakuni endapo atajipendekeza kwa hali yoyote ile kumtafuta Carolina.
“Hapana,” alijishtukia akiweweseka kwa sauti ya ukali mbele ya mteja wake mkubwa, Salima ambaye muda mwingine alikuwa akimsemesha huku akimkabidhi simu yake ya mkononi kwa ombi la huduma ya kuchajisha lakini bila mafanikio.
“Ooh! Samahani sana Salima, ulikuwa unasema nini?” Dedan aligutuka kutoka katika vita ya nafsi na kushusha pumzi ndefu akimwomba Salima arejee maongezi yake ya awali.
“Dedan, mzima kweli leo wewe?” Salima aliuliza baada ya kugundua hali ya kubabaika ya Dedan.
“Mi mzima tu...lete stori,” kwa uchangamfu Dedan aliongea kiasi cha kumshawishi Salima aamini kwamba kila kitu kilikuwa sawasawa.
“Hata hivyo, siku zote ni nzuri kwa Dedan, ni kama anaishi katika ulimwengu wa pekee, japo ni maskini mwenzangu, anaonekana haumizwi na kitu. Shida hizi anazichukulia kama changamoto kwa kupigana kwa nguvu zake zote kupata maendeleo tofauti na vijana wengi wa rika lake.
“Kweli ninatamani sana niwe na mwanaume kama huyu. Hapana si kama, bali ni huyu huyu…Mh! Lakini namwogopa kumuanza, sijui atanichukuliaje? Mtu mwenyewe ni mwingi wa shughuli! Ila nitamwambia kesho asubuhi nikija kuchukua simu yangu.
“Nitamtumia meseji nzuri ya mapenzi. Nimejaribu kumfanyia mambo mengi ilimradi azisome hisia zangu, lakini mtu mwenyewe wala haoni,” aliwaza Salima huku akiwa amesimama na kujichekesha na kuweka tabasamu pana mbele ya Dedan aliyekuwa akimtazama tu bila kuona chochote.
Mawazo yake yalikuwa mbali, kama vile ana macho lakini haoni na ana masikio lakini hasikii.
“Usiku mwema Dedan,” aliongea Salima kwa huruma na upole baada ya kugundua ameshindwa kulinasa windo lake kwa siku hiyo.
Mbinu alizofundishwa na kungwi wake, Bi. Hamdani wa Masasi hazikufua dafu mbele ya Dedan.
Alitamani amrukie na kumbusu kwa nguvu ili amjulishe hisia zake, lakini alihofia akiamini ataonekana msichana malaya kama si aliyekosa maadili mema.
“Nitasubiri nafasi yangu, sitaki niharibu yote niliyoyaanza. Kwa Dedan nitakuwa mwanamke mstaarabu, mwema na mwaminifu daima naamini atanipenda tu,” alijiapiza na kujiondokea zake moyoni akilia na kumlaumu mwanaume huyo kwa kutojua windo lake.
“Usiku mwema Dedan…usiku mwema mpenzi wangu...” chochote asichokisema kwa sauti kumwambia Dedan moja kwa moja, aliamua kukimalizia kwa kuongea kwa sauti ndogo akitumaini ipo siku atamjibu na kumuuliza mambo mengi wakiwa kama mke na mume.
Baada ya kuhakikisha amemaliza na kuweka vizuri kila kitu, Dedan aliitazama saa juu ya kioo cha simu yake iliyoonesha namba ishirini na moja, ikiashiria saa tatu usiku kwa urekebisho wa saa ishirini na nne za siku moja.
Alifunga vyema ofisi yake kisha akatokomea huko vichochoroni ambako aliwahi kusikia vinauzwa hivyo vinavyopoteza mawazo, eti pombe!
“Hakuna muda mzuri wa kuamua kuwa chakari kama huu,” Dedan alijisukuma kwa mara ya kwanza kwenye vilabu vya pombe za kienyeji.
Aliamini atalewa kwa gharama ndogo sana huku akifanikiwa angalau kuvuka makali ya upweke kwa usiku huo wa kwanza akilala akiwa anajua kabisa hataishi na Caro wake tena.
***
Asubuhi aliamka na kujinyoosha na kupiga miayo mfululizo. Alionekana mwingi wa uchovu kutokana na pombe kali za jana yake. Ghafla alijishangaa machozi yakimbubujika. Alitaka kuamka, lakini akashindwa. Jasho jingi lilimtoka mwilini huku mapigo ya moyo yakienda kwa kasi ya ajabu. Kama mzigo alidondoka chini na kupoteza fahamu.
ITAENDELEA KESHO MUDA KAMA HUU.
USISAHAU KULIKE, COMMENT NA KUSHARE mnipe nguvu nipost tena Karibu ulike page yetu ya www.facebook.com/bongochoice ili tuburudike na simulizi...
Credit : 2jiachie
ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA
TARATIBU zimwi la upweke likamzonga na kuushinda kirahisi ustahimilivu wa moyo wa Dedan. Kama mfungwa kwa mawazo yake akajikuta hajielewi kabisa. Kichwani akiwaza mara ya kwanza alipoongea na Caro kwa njia ya simu…
ENDELEA SASA...
“Mungu wangu! Msichana mrembo wa ajabu huyu,” alisema moyoni Dedan. Akakumbuka pia alipoamua kumfungulia kurasa mpya za mapenzi ndani ya kuta za moyo wake.
Alikumbuka vyema kila zuri walilofanya pamoja, wakicheza baharini na kurushiana mito kitandani. Walilishana chakula na kubusiana kimahaba.
Lakini hayo yote yalitoweka ghafla baada ya kukumbuka sauti kali ya Carolina kwenye simu ikimtosa bila huruma na pasipokuwa na sababu yoyote. Akasikia sauti nyingine ya mwanaume wake wa sasa ikimchimba mkwara kwamba atakiona cha mtemakuni endapo atajipendekeza kwa hali yoyote ile kumtafuta Carolina.
“Hapana,” alijishtukia akiweweseka kwa sauti ya ukali mbele ya mteja wake mkubwa, Salima ambaye muda mwingine alikuwa akimsemesha huku akimkabidhi simu yake ya mkononi kwa ombi la huduma ya kuchajisha lakini bila mafanikio.
“Ooh! Samahani sana Salima, ulikuwa unasema nini?” Dedan aligutuka kutoka katika vita ya nafsi na kushusha pumzi ndefu akimwomba Salima arejee maongezi yake ya awali.
“Dedan, mzima kweli leo wewe?” Salima aliuliza baada ya kugundua hali ya kubabaika ya Dedan.
“Mi mzima tu...lete stori,” kwa uchangamfu Dedan aliongea kiasi cha kumshawishi Salima aamini kwamba kila kitu kilikuwa sawasawa.
“Hata hivyo, siku zote ni nzuri kwa Dedan, ni kama anaishi katika ulimwengu wa pekee, japo ni maskini mwenzangu, anaonekana haumizwi na kitu. Shida hizi anazichukulia kama changamoto kwa kupigana kwa nguvu zake zote kupata maendeleo tofauti na vijana wengi wa rika lake.
“Kweli ninatamani sana niwe na mwanaume kama huyu. Hapana si kama, bali ni huyu huyu…Mh! Lakini namwogopa kumuanza, sijui atanichukuliaje? Mtu mwenyewe ni mwingi wa shughuli! Ila nitamwambia kesho asubuhi nikija kuchukua simu yangu.
“Nitamtumia meseji nzuri ya mapenzi. Nimejaribu kumfanyia mambo mengi ilimradi azisome hisia zangu, lakini mtu mwenyewe wala haoni,” aliwaza Salima huku akiwa amesimama na kujichekesha na kuweka tabasamu pana mbele ya Dedan aliyekuwa akimtazama tu bila kuona chochote.
Mawazo yake yalikuwa mbali, kama vile ana macho lakini haoni na ana masikio lakini hasikii.
“Usiku mwema Dedan,” aliongea Salima kwa huruma na upole baada ya kugundua ameshindwa kulinasa windo lake kwa siku hiyo.
Mbinu alizofundishwa na kungwi wake, Bi. Hamdani wa Masasi hazikufua dafu mbele ya Dedan.
Alitamani amrukie na kumbusu kwa nguvu ili amjulishe hisia zake, lakini alihofia akiamini ataonekana msichana malaya kama si aliyekosa maadili mema.
“Nitasubiri nafasi yangu, sitaki niharibu yote niliyoyaanza. Kwa Dedan nitakuwa mwanamke mstaarabu, mwema na mwaminifu daima naamini atanipenda tu,” alijiapiza na kujiondokea zake moyoni akilia na kumlaumu mwanaume huyo kwa kutojua windo lake.
“Usiku mwema Dedan…usiku mwema mpenzi wangu...” chochote asichokisema kwa sauti kumwambia Dedan moja kwa moja, aliamua kukimalizia kwa kuongea kwa sauti ndogo akitumaini ipo siku atamjibu na kumuuliza mambo mengi wakiwa kama mke na mume.
Baada ya kuhakikisha amemaliza na kuweka vizuri kila kitu, Dedan aliitazama saa juu ya kioo cha simu yake iliyoonesha namba ishirini na moja, ikiashiria saa tatu usiku kwa urekebisho wa saa ishirini na nne za siku moja.
Alifunga vyema ofisi yake kisha akatokomea huko vichochoroni ambako aliwahi kusikia vinauzwa hivyo vinavyopoteza mawazo, eti pombe!
“Hakuna muda mzuri wa kuamua kuwa chakari kama huu,” Dedan alijisukuma kwa mara ya kwanza kwenye vilabu vya pombe za kienyeji.
Aliamini atalewa kwa gharama ndogo sana huku akifanikiwa angalau kuvuka makali ya upweke kwa usiku huo wa kwanza akilala akiwa anajua kabisa hataishi na Caro wake tena.
***
Asubuhi aliamka na kujinyoosha na kupiga miayo mfululizo. Alionekana mwingi wa uchovu kutokana na pombe kali za jana yake. Ghafla alijishangaa machozi yakimbubujika. Alitaka kuamka, lakini akashindwa. Jasho jingi lilimtoka mwilini huku mapigo ya moyo yakienda kwa kasi ya ajabu. Kama mzigo alidondoka chini na kupoteza fahamu.
ITAENDELEA KESHO MUDA KAMA HUU.
USISAHAU KULIKE, COMMENT NA KUSHARE mnipe nguvu nipost tena Karibu ulike page yetu ya www.facebook.com/bongochoice ili tuburudike na simulizi...
Post a Comment